Katibu Mkuu wa Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo, Gerson Msigwa ametambia mafanikio ambayo Tanzania imeonyesha katika michezo miaka ya hivi karibuni.
Akizungumza katika hafla ya kuzichangia timu za taifa inayofanyika katika Hoteli ya Johari Rotana, Msigwa amesema kuwa Tanzania ya sasa ni tishio michezoni.
"Tunamshukuru Rais kwa mchango wake mkubwa kwenye sekta ya michezo. Mafanikio tunayopata hatujawahi kuyapata katika nyakati nyingine zote," amesema Msigwa.
Msigwa amesema kuwa anaipongeza kamati ya hamasa iliyoundwa kwa ajili ya kuhamasisha timu za taifa, imefanya kazi kubwa na anaamini itakuwa na mchango katika maendeleo ya michezo.
"Kamati ya hamasa ina wiki moja lakini imefanya mambo makubwa sana, tumefanya Harambee hii kwa ajili ya kuchagiza maendeleo hayo," alisema Msigwa