Tue, 23 Apr 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Winga wa Simba SC, Willy Esomba Onana ataondoka ndani ya klabu hiyo mwishoni mwa msimu huku SuperSport united wakiwa tayari wameonyesha nia ya kutaka kumsajili.
Taarifa zinasema kuwa Simba sc wanataka kiasi Cha $75k ambayo ni sawa na milioni (194,550,976.00) za kitanzania ili kumruhusu aondoke ndani ya klabu ya Simba SC.
Willy Onana yuko tayari kuondoka klabuni hapo, klabu itatoa taarifa rasmi mara tu makubaliano yatakapofikiwa na Super Sports United ya nchini Afrika Kusini.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live