Fri, 18 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mbali ya Brighton, West Ham pia inatajwa ni timu nyingine kutoka England inayohitaji huduma ya kiungo wa Ajax, Mohammed Kudus katika dirisha hili na inataarifiwa kuwa iko katika hatua nzuri kuliko wapinzani wao Brighton.
West Ham inataka huduma ya fundi huyu kama mbadala wa staa wao kutoka Brazil, Lucas Paqueta, 25, anayehusishwa na Manchester City.
Kudus anadaiwa kuomba kuondoka Ajax kwenye dirisha hili na huko nyuma aliwahi pia kuhusishwa na Manchester United akajiunge na Kocha Eric Ten Hag.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live