Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

West Ham kumpiga Faini Zouma mshahara wa wiki 2

Kourt Zuma Fined Beki wa West Ham, Kourt Zouma

Thu, 10 Feb 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Klabu ya West Ham United imethibitisha kwamba mchezaji wake Kurt Zouma ameadhibiwa kwa kupigwa faini ya kukatwa mshahara wa wiki mbili kutokana na tukio la unyanyasaji wa wanyama.

Klabu ya West Ham imesema kuwa inaheshimu na kuisaidia RSPCA kwenye upelelezi wao baada ya video ya Kurt Zouma kusambaa ikimuonysha akimuadhibu paka, na faini atayokatwa ya £250k itapelekwe kwenye taasisi ya haki za wanyama.

West Ham walitoa waraka wao kuhusu tukio hilo, “tunaweza kuthibitisha kuwa klabu inaisaidia RSPCA kwenye upelelezi kuhusu tukio alilolifanya Kurt Zouma, ambaye video yake imekuwa ikisambaa mtandaoni wiki hii.

“Kurt na klabu tunashirikiana kwa pamoja kwenye upelelezi na mchezaji amekubali kushirikina kwenye hatua zote muhimu atakzohitajika ikiwemo kuwafikisha paka wake wawili kwa RSPCA kwa ajiri ya vipimo.

“West Ham tungependa kurudia tena kukemea kitendo cha Kurt na kuweka sawa jambo hili kuwa tutaendelea kulishughulikia kwa ukaribu zaidi, japokuwa tunaamini sasa ni muhimu kuwaruhusu RSPCA kuendelea na uchunguzi zaidi wa hatua zinazofuata.”

Chanzo: www.tanzaniaweb.live