Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally amesema kuwa mpaka sasa hajapata taarifa rasmi kuhusu iwapo wataendelea kuwa na kiungo wao mshambuliaji, Clatous Chota Chama ama ataondoka klabuni hapo.
Chama ambaye mkataba wake unamalizika Juni 30, 2024 ndani ya Yanga, anatajwa kuwa ameshasaini mkataba wa mwaka mmoja na watani zao, Yanga SC ambao wamekuwa wakimuwinda kwa miaka mingi.
“Kuhusu Mwamba wa Lusaka, Clatous Chota Chama nikiri kwamba sijapata mwongozo mpya kuhusu yeye. Taarifa niliyo nayo ni kwamba anamaliza mkataba wake mwishoni mwa msimu huu na bado sijaambiwa kama ameongeza mkataba ama hajaongeza mkataba na kama tunaendelea naye ama hatutaendelea naye,” amesema Ahmed.