Mon, 2 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk Damas Ndumbaro ameikaribisha klabu ya Al Ahly ya Misri ije kuwekeza katika sekta ya michezo nchini Tanzania kwa kufungua akademi ya michezo ili kukuza na kuendeleza vipaji vya wanamichezo.
Dk Ndumbaro ameikaribisha klabu hiyo namba moja Afrika hivi karibuni alipofanya ziara kuona uwekezaji mkubwa uliofanywa na timu hiyo katika jiji la Cairo, nchini Misri.
Timu hiyo pia inamiliki kituo cha Gezira Center ambacho kinaendesha viwanja vya michezo mbalimbali ikiwemo soka, mpira wa wavu, mpira wa netiboli, gofu na riadha.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live