Thu, 19 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Waziri Mkuu wa Ivory Coast, Robert Beugre Mambe, amechukua jukumu la Wizara ya michezo wakati nchi ikijiandaa kuwa mwenyeji wa Michuano ya Africa Cup of Nations (AFCON).
Hatua hiyo imekuja wakati kukiwa na wasiwasi kuhusu utayari wa nchi hiyo kusimamia mashindano ya AFCON yatakayoanza mwezi Januari.
Waziri wa zamani wa Michezo wa Ivory Coast alifukuzwa kazi wiki iliyopita huku kukiwa na ukosoaji juu ya ubora duni wa Uwanja mkuu nchini humo. Nchi hiyo ina viwanja sita ambamo mechi za AFCON zinatarajia kuchezwa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live