"Kwa aina ya washambuliaji wazawa tulionao unaweza kusema Waziri Jr Shentembo ndio top kulingana na ubora aliyoonyesha msimu huu akiwa na goli 12.
Msimu ule wakati anaenda Yanga akitokea Mbao FC hakufanya vizuri kwa sababu pia Yanga ile ilikuwa unga unga kwa sababu haikuwa na mafundi kama ilivyo Yanga hii ya Masta Miguel Gamondi.
Naamini kama viongozi wa Yanga watafanya movement ya kumsajili tena Waziri Junior Shentembo basi huenda akafanya vizuri kulingana na mseto wa wachezaji wazuri uliopo Yanga kwa sasa.
Yanga ya sasa inatengeneza nafasi nyingi,inafunga magoli mengi. Kwa aina ya uchezaji wa Waziri Jr huenda akafanya vizuri zaidi ya alichokifanya pale KMC" Mbwana Mshindo.