Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wawili Coastal Union kuikosa Azam FC

Kocha Coastal Union Matumaini Kibao Safari Ya Dodoma Wawili Coastal Union kuikosa Azam FC

Thu, 1 Jun 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kocha Mkuu wa Coastal Union, Fikiri Elias, amethibitisha kuwakosa nyota wake wawili, Khatib Kombo na Gerald Gwalala, kwenye mchezo wao dhidi ya Azam FC unaotarajiwa kupigwa Juni 6, mwaka huu kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

Elias amesema: “Wachezaji wote waliokuwa majeruhi awali wamerejea katika hali yao ya kawaida na wanaendelea kujiwinda dhidi ya Azam, isipokuwa tutawakosa nyota wetu wawili ambao ni Khatib Kombo na Gerald Gwalala.

“Kombo ana matatizo ya kifamilia ambayo ameenda kuyasuluhisha lakini kwa upande wa Gwalala tutamkosa kwenye mechi takriban tatu kutokana na adhabu yake ya kadi.

“Tuna mechi ngumu sana mbele yetu, Azam ni wapinzani wakubwa sana lakini mechi hii wataicheza kwetu na siku zote mcheza kwao hutunzwa hivyo lazima tuhakikishe kuwa tunapata ushindi na sapoti ya kutosha kutoka kwa wadau na mashabiki wa Coastal Union.”

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: