Thu, 15 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo (uwanja wa nyumbani wa JKT Tanzania) una uwezo wa kuingiza mashabiki 4,000 tu.
Kwa mujibu wa Ofisa Habari na Mawasiliano JKT Tanzania, Masau Bwire uwanja huo bado upo kwenye ujenzi wa majukwaa lakini kwa sasa jukwaa linalotumika ni moja tu.
Jukwaa hilo lina uwezo wa kuchukua mashabiki 200 walioketi, kwa mchezo wa leo jukwaa hili litatumiwa na watu maalum. Mashabiki wengine wote watakuwa kwenye eneo la mzunguko ambako watasimama.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live