Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Watatu Yanga wajiuzulu, wawili wasimamishwa

100519 Pic+yanga Watatu Yanga wajiuzulu, wawili wasimamishwa

Sat, 28 Mar 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

HALI ndani ya Yanga sio shwari baada ya wajumbe watatu wa Kamati ya Utendaji kutangaza kujiuzulu nafasi zote walizokuwa nazo klabu, huku wengine wawili wakisimamishwa kwa utovu wa nidhamu, ikiwa siku chache tangu Kampuni ya GSM kutishia kusitisha huduma zake klabuni.

Waliotangaza kujiuzulu na maamuzi yao kukubaliwa na kikao cha Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo ni Rodgers Gumbo, Said Kambi na Shija Richard, huku waliosimamishwa kwa muda usiojulikana ni pamoja na vigogo wa Kamati ya Usajili, Frank Kamugisha na Salim Rupia.

Wajumbe hao wamechukua maaamuzi hayo kutokana na kikao kizito klilichofanyika kwa muda wa siku mbili kuanzia jana na leo, ikiwa ni siku chache tangu GSM ambayo ni moja ya wadhamini wa klabu hiyo kuandika barua kusitisha huduma walizokuwa wakizifanya nje ya mkataba wao.

Inaelezwa wajumbe hao hawakuwa wakiiva na kampuni hiyo iliyokuwa ikisimamia ishu za usajili, kuhudumia kambi na kulipa posho na mishahara ya wachezaji kwa kilichoelezwa ni kuingilia majukumu ya kamati hiyo na kuwachefua wanachama wa klabu hiyo wakihofia Yanga kurudi kwenye kutembeza bakuli.

Jioni uongozi wa klabu hiyo iliyo chini ya Mwenyekiti wake, Dk. Mshindo Msolla umetoa taarifa rasmi juu ya maamuzi ya kamati hiyo ya utendaji sambamba na kueleza wameijibu barua ya GSM walioandikiwa Machi 24 mwaka huu.

Taarifa hiyo rasmi ya Yanga ilitiwa saini na Dk Mshindo ikifafanua kuwa wameridhia kina Gumbo kujiuzulu.

Pia Soma

Advertisement
Awali ilielezwa wajumbe hao walishinikizwa kujiuzulu kwa nia ya kutuliza upepo mbaya na kwenye taarifa zao, Gumbo na Shija wamesema wanaamini muda utakuja kusema baadaye, licha ya kwamba wameridhia wenyewe kuachia ngazi kwa vile Yanga ni kubwa kuliko wao na wataendelea kuwa wanachama waaminifu wa Jangwani.

Chanzo: mwananchi.co.tz