Thu, 30 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mabingwa watetezi, Manchester City wamezidi kuwaacha mbali wapinzani baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji, Brentford City usiku wa Jumatano Uwanja wa Brentford Community, Brentford, Middlesex.
Sifa zimuendee mfungaji wa bao hilo pekee, Phil Foden dakika ya 16 akimalizia kazi nzuri ya Kevin de Bruyne kumchambua kipa Alvaro Fernandez.
Ushindi huo unaifanya Manchester City imalize mwaka kileleni mwa Ligi Kuu ya England kwa pointi zake 50, nane zaidi ya mabingwa wa Ulaya, Chelsea wanaofuatia baada ya wote kucheza mechi 20.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live