Thu, 8 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Leo Alhamisi ni siku nyingine tena, timu ya Young Africans SC inashuka dimbani kumenyana na Mashujaa FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC utakaochezwa Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.
Mchezo huo utaanza majira ya saa 1:00 usiku ambapo tayari viingilio vimewekwa hadharani na tiketi kuanza kuuzwa tangu jana.
Viingilio vya mchezo ni Tsh 20,000 Jukwaa la V.I.P A, Tsh 10,000 (V.I.P B) na Mzunguko Tsh 5,000.
Timu hiyo leo itaingia uwanjani ikiwa inaongoza kunako msimamo wa Ligi Kuu ya NBC baada ya kukusanya pointi 34.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live