Wanajeshi walio na silaha wamevamia hoteli waliyofikia Timu ya Taifa ya Tanzania, "Taifa Stars" katika mji wa Antananarivo nchini Madagascar.
Wanajeshi hao wameweka kambi katika korido za vyumba vya Wachezaji wa Stars wakidai kuwa kuna kesi ya uwepo wa viashiria vya kuwepo kwa wagonjwa wa Corona miongoni mwa wachezaji wa Stars.
Taifa Stars ipo nchini Madagascar kwa ajili ya mchezo wao dhidi ya timu ya Taifa ya Madagascar kuwania kufuzu kwa Fainali za Kombe la Dunia zitakazochezwa Qatar 2022.
Mchezo huo ni wa kukamilisha makundi na ni wa kundi J, ambalo linaongozwa na Benin mpaka sasa.
Soldiers have invaded Tanzania team hotel in Antananarivo and stationed at players’ rooms corridor with guns ahead of World Cup Qualifiers match against hosts Madagascar. Soldiers claimed that there are Covid-19 cases in Tanzania team @FIFAWorldCup @CAF_Online pic.twitter.com/ajw18agCMl
— TFF TANZANIA (@Tanfootball) November 14, 2021