Waliomleta Manzoki kwenye uchaguzi na kuahidi atajiunga na Simba wamebaki, Mwalimu ambaye zaidi ya mechi 26 hajapoteza na kafungwa mechi moja tu ya ligi na kuwapa ngao waliyokosa misimu miwili kafukuzwa.
Sipingani Mwalimu kufukuzwa ila Viongozi nao wawajibike, watoke nao! Kuipenda timu sio kumfukuza Mwalimu bali kuipenda zaidi ni wao pia kujitafakari na kupisha ofisini, ni uwajibikaji kuwa kwa pamoja tumefeli.
Sayansi ya mpira inatuonesha timu inapaswa kuanza upya, kuanzia huko GYM, ofisini na uwanjani, timu inataka njia mpya ambayo naona bado haijafikiwa mpaka sasa, Kocha wa ngapi ndani ya misimu miwili na nusu?