Nyota wa zamani wa soka wamejitokeza kwa wingi katika hafla ya tuzo za TFF inayoendelea katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam.
Idadi kubwa ya wachezaji hao ni wale waliochezea Simba na Yanga miaka ya nyuma ingawa wapo waliowahi kutamba katika timu nyingine
Mjumbe wa kamati ya utendaji ya TFF, James Mhagama aliyewahi kuchezea Majimaji ya Songea ni miongoni mwa nyota wa zamani waliojitokeza katika hafla hiyo
Nahodha wa zamani wa Yanga, Ally Mayay naye pia yupo katika hafla hii huku pia akiwepo nyota wa zamani wa Simba, Abdallah Kibaden aliyeshinda tuzo ya gwiji wa soka.
Pia wapo Abeid Mziba, Ramadhan Kampira, Madata Lubigisa, Hery Morris na Mohamed Mwameja
Wengine ni Mohamed Muharami, Jemedari Said na Katibu Mkuu wa TFF, Wilfred Kidao aliyewahi kuchezea Simba