Klabu ya USM Algiers ambao ni Mabingwa watetezi wa Kombe la Shirikisho Afrika wamepigwa Faini na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kutokana na vitendo vyao viouvu walivyovifanya katika mchezo wa Fainali dhidi ya Yanga.
Habari hii ni kama haijapewa uzito mkubwa na vyombo vya habari hapa nchini jambo lililomfanya Mkurugenzi wa Sheria wa Yanga, Wakili Simon Patrick kutupa dongo kwa Wanahabari.
Kupitia Ukurasa wake wa Instagram Wakili Simon Patrick amandika;
"USMA Alger wamepigwa bonge la fine kwa matukio waliyoyafanya kwenye mchezo wa fainali dhidi ya Young Africans Sports Club, habari hii haijavuja popote, hii inakufundisha nini?
When you choose popularity over integrity, it is called “Lack of Proficiency” - Simon Patrick, Mwanasheria wa klabu ya Yanga SC.