Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wakala afunguka Che Malone kusepa Simba

WhatsApp  Che Fondoh Malone.jpeg Wakala afunguka Che Malone kusepa Simba

Wed, 10 Apr 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Wakala wa Beki wa Klabu ya Simba, Che Malone, Amadou Fontem Tigana, amesema beki huyo hajasema kuwa haipendi Simba na wala hajasema kuwa anataka kuondoka Simba, bali watu wamemtafsiri vibaya mchezaji huyo.

Tigana ameyasema hayo wakati akizungumza na ITV kwa njia ya simu, ambapo amesisitiza kuwa taarifa hizo ni uzushi kwani ametafsiriwa vibaya baada ya kusema kuwa atacheza Kwa juhudi ili klabu kubwa kama Simba zimnunue.

Ufafanunuzi huo wa Tigana unafuata, baada ya kusambaa kwa taarifa kuwa mchezaji huyo amefanya mahojiano kuwa hatakuwa sehemu ya kikosi cha Simba msimu ujao na kwamba tayari ameandika barua ya kuondoka Simba na kwamba anatala akatafute changamoto kwenye timu kubwa.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live