Tue, 31 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wajumbe wa Chama cha soka Wilaya ya Ubungo (UFA) wametangaza kugomea kushiriki uchaguzi kwa kile wanachodai ni ukiukwaji wa utaratibu wa uchaguzi
Kwenye mkutano na waandishi wa habari wajumbe hao wamedai mchakato wa kupendekeza majina ya wagombea una mashaka baada ya majina ya baadhi ya wagombea kukatwa na kuachwa jina moja kwenye kila nafasi .
Wagombea nafasi ya mwenyekiti walikuwa wanne (4) lakini watatu wamekatwa limebaki jina moja , wagombea nafasi ya ujumbe walikuwa watano ,wanne wamekatwa amebaki mmoja .
Chanzo: www.tanzaniaweb.live