Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wafahamu mastaa 10 wa soka ambao hawana tattoo mwilini mwao

Cristiano Ronaldo Madrid Career Wafahamu mastaa 10 wa soka ambao hawana tattoo mwilini mwao

Mon, 16 Oct 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mpira wa Miguu ni sehemu ya kaaida ya maisha ya wanadamu, mashabiki na wachezaji huwa na hisia moja ya kushangilia ushindi na kuumia kipindi timu yao pendwa inapofungwa. Hali hii inanifanya kurudi darasani na kukumbuka somo moja linaitwa Media and Culture, yaani Utamadni na Vyombo vya Habari.

Kwenye somo hilo nilisoma namna ambavyo Utamaduni wa jamii unavyopaswa kutunzwa na kurithishwa kupitia Vyombo vya Habari, moja ya sehemu niliyoipenda sana ni utamaduni wa wachezaji wa soka maisha yao yanavyoathiri mashabiki zao. Mfumo wa maisha kama kuchora Tattoo, mtindo wa nywele, maisha ya nje ya uwanja.

Leo nashusha Jamvi la mastaa wa soka 10 wasiokuwa na Tattoo mwilini mwao:

Harry Kane Ni mchezaji wa Bayern Munich aliyejiunga akitokea Tottenham ya Uingereza akiwa ndiyo mfungaji bora wa klabu hiyo, Kane anasema kwamba kipindi akiwa mtoto baba yake alimkatalia kuchora Tattoo na mpaka sasa haoni ulazima wa kufanya hivyo.

Robert Lewandowski Alizaliwa mnamo Agosti 21, 1988. Ni nahodha wa timu ya taifa yaPoland na mshambuliaji namba moja wa FC Barcelona, licha ya mafanikio yake yote Lewa amekataa kabisa kuchora tattoo kwene mwili wake bila kutaja sababu.

David Luiz David Luiz alizaliwa Aprili 22, 1987. Ni mwanasoka wa kulipwa wa Brazil ambaye anachezea Flamengo.

Luiz ni Mkatoliki mwaminifu kama Waamerika wengi wa Kusini lakini kwake yeye suala la Tattoo mwilini mwake ni mwiko. Katika ubora wa Luiz bila shaka alikuwa anakupa sana pesa.

Gareth Frank Bale Alizaliwa Julai 16, 1989. Ni mchezaji wa kandanda wa Wales ambaye anacheza kama winga kwenye klabu ya Los Angeles FC na timu ya taifa ya Wales.

Kwa mujibu wake aliwahi kusema hana tattoo yoyote kwa sababu bab yake hajamruhusu achore.

Kylian Mbappe Lottin Alizaliwa Desemba 20, 1998. Ni mchezaji wa timu ya taifa ya Ufaransa ambaye anacheza kama mshambuliaji wa PSG kwenye Ligue 1.

Mbappe amekataa kujichora tattoo mwilini pengine kwa sababu ni mdogo sana kuweza kujichora, lakini hajatoa sababu rasmi ya kutokuwa na tattoo.

Paul Pogba Mchezaji huyu wa kimataifa wa Ufaransa hana Tattoo yeyote kwenye mwili wake kwa madai ya kwamba Imani yake ya Kiislam hairuhusu kufanya hivyo.

N’Golo Kante Amezaliwa Machi 29, 1991. Ni mchezaji wa Kimataifa wa Ufaransa na anakipiga kwenye Ligi kuu ya Saudia kwenye klabu ya El-Ettihad. Mwili wake hauna tattoo na hataki kabisa kuchora.

Sadio Mane Amezaliwa katika familia duni huko Senegal lakini kwa sasa ni tajiri wa kutupwa akiwa na mafanikio ya soka kama tuzo ya mchezaji bora wa kiume wa Afrika. Mafanikio huja na juhudi, wekeza juhudi zako kwa kubashiri Meridianbet upate kushinda.

Mane ni miongoni mwa wanasoka wasiokuwa na Tattoo kwenye mwili wake, kwakuwa dini yake ya Kiislam hairuhusu muumini kuchora tattoo ni haramu.

Mohamed Salah Mohamed Salah Hamed Mahrous Ghaly ni mchezaji wa kimataifa wa Misri kwa Mapharao, lakini pia anakipiga katika EPL na Majogoo klabu ya Liverpool. Salah ni moja ya wachezaji wasiokuwa na Tattoo moja ya sababu ni Imani yake hairuhusu mambo hayo.

Cristiano Ronaldo. Cristiano Ronaldo dos Santos Aveiro amezaliwa Februari 5, 1985 huko Ureno, ni mshindi wa Ballon D’or 5 na akiwa ameshinda mataji 33, ya Ligi 7, Uefa Champions League 5, UEFA European Championship na UEFA Nations League.

Katika mwili wake huwezi kukuta tattoo kwa kile alichobainisha kwamba “Huchangia damu, hivyo kuchora tattoo kutamchukua muda mrefu kurejesha seli na chembe za damu katika hali yake ya kawaida”

Chanzo: www.tanzaniaweb.live