Mon, 16 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Baadhi ya wachezaji na sehemu ya benchi la ufundi la Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) ambao baada ya kumalizika mechi ya jana ya Kirafiki ya Kimataifa dhidi ya Sudan, walienda kufanya ibada ya Umrah katika msikiti mtukufu wa Makkah ambao upo nchini Saudi Arabia.
Kutoka mji wa Al Taif ambako mechi ilichezwa kwenda mji ambao msikiti huu unapatikana ni mwendo wa saa moja tu kwa gari.
Mechi hiyo kati ya Tanzania na Sudan iliyopigwa nchini Saudi Arabia ilimalizika kwa sare ya bao 1-1, bao la Tanzania likifungwa na Sospeter Bajana.
Neno moja la kheri kwao kwa ibada hii ya Umrah.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live