Wed, 13 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wachezaji wa klabu ya Napoli wamekosa zaidi ya €10 Million [ TZS Billion 28] ambayo waliahidiwa na mmiliki wa klabu hiyo Aurelio De Laurentiis kama wangefanikiwa kuiondosha Barcelona kwenye hatua ya 16 ya Ligi ya mabingwa Ulaya.
"Niliweka zaidi ya Dola Million 10." alisema Aurelio De Laurentiis
Napoli ilitoa sare mchezo wa kwanza ikiwa nyumbani [1-1] na jana wakiwa Camp Nou walipoteza kwa goli 3-1 na hivyo klabu hiyo kuondoshwa kwa idadi ya magoli 4-2.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live