Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wachezaji 6 Man U akiwemo Pogba kutimka Januari

63f5adf10e67c47f Wachezaji 6 Man U akiwemo Pogba kutimka Januari

Sun, 5 Dec 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Baadhi ya wachezaji nyota wa Man United wanatarajiwa kuondoka ndani ya klabu hiyo kufuatia kuteuliwa kwa kocha mpya Ralf Rangnick.

Edinson Cavani ndiye anaongoza kwenye orodha hiyo ya wachezaji wa United ambao watahamia katika vilabu vingine huku mkataba wake ukikaribia kukatika msimu wa joto Jesse Lingard, Digo Dalot, na Anthony Martial pia wanaaminika kuwa na mpango wa kuondoka.

Edison Cavani anaongoza kwenye orodha ya wachezaji wa Man United ambao huenda wataondoka klabuni miezi michache zijazo baada ya kuteuliwa kwa Ralf Rangnick kuwa meneja mpya.

Rangnick alikabidhiwa mikoba hiyo Jumatatu na kumrithi Ole Gunnar Solskjaer ambaye alifutwa kazi hivi majuzi na klabu hiyo ya Manchester.

Mirror UK sasa inaripoti kwamba kuwasili kwa Rangnick huenda kutachochea wachezaji kadhaa kuondoka, huku Mjerumani huyo akitarajiwa kufanyia timu yake mabadiliko ambayo imekuwa na masaibu mengi msimu huu.

Inaripotiwa kuwa tayari mkufunzi huyo mwenye umri wa miaka 63, amewasilisha bajeti ya pauni 100 milioni ya kupiga jeki kikosi chake kuelekea msimu wa dirisha la uhamisho Januari.

Masajini wapya ugani Old Trafford bila shaka watachochea baadhi ya wachezaji kuchujwa huku sita wakitazamiwa kuondoka.

Cavani, ambaye amesalia na miezi sita katika mkataba wake wa sasa, anaongoza orodha ya wachezaji wanaotazamiwa kuondoka, huku akidaiwa kuyoyomea Barcelona.

Paul Pogba na Jesse Lingard pia wanaaminikan kuwa na hamu ya kuondoka huku Pogba akikataa kusaini mkataba mpya.

Lingard, kwa upande wake amepungukiwa kimchezo sabab ya ushindani, winga huyo akionekana kuondoka kama mchezaji wa bwerere iwapo United watashindwa kumpata mnunuzi wake Januari.

Wengine ni Anthony Martial, Diogo Dalot, na Donny van de Beek.

Licha ya ubabe wake Old Trafford, Martial ameshindwa kutimiza wajibu wake na sasa atatupwa sokoni United wakijaribu kurejesha pesa walizolipa Monaco kupata huduma zake.

Dalot, naye ameshindwa kuonyesha maana yake tangu kusajiliwa kwake na Mashetani Wekundu chini ya ukufunzi wa Jose Mourinho akitokea Porto mwaka 2018, akishiriki michezo 24 pekee za EPL tangu kutua kwake.

Wakati huo huo Van de Beek, amekuwa na wakati mgumu Theatre of Dreams, akisugua benchi msimu mzima akiwa na United.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke