Baadhi ya wachezaji nyota wa Man United wanatarajiwa kuondoka ndani ya klabu hiyo kufuatia kuteuliwa kwa kocha mpya Ralf Rangnick.
Edinson Cavani ndiye anaongoza kwenye orodha hiyo ya wachezaji wa United ambao watahamia katika vilabu vingine huku mkataba wake ukikaribia kukatika msimu wa joto Jesse Lingard, Digo Dalot, na Anthony Martial pia wanaaminika kuwa na mpango wa kuondoka.
Edison Cavani anaongoza kwenye orodha ya wachezaji wa Man United ambao huenda wataondoka klabuni miezi michache zijazo baada ya kuteuliwa kwa Ralf Rangnick kuwa meneja mpya.
Rangnick alikabidhiwa mikoba hiyo Jumatatu na kumrithi Ole Gunnar Solskjaer ambaye alifutwa kazi hivi majuzi na klabu hiyo ya Manchester.
Mirror UK sasa inaripoti kwamba kuwasili kwa Rangnick huenda kutachochea wachezaji kadhaa kuondoka, huku Mjerumani huyo akitarajiwa kufanyia timu yake mabadiliko ambayo imekuwa na masaibu mengi msimu huu.
Inaripotiwa kuwa tayari mkufunzi huyo mwenye umri wa miaka 63, amewasilisha bajeti ya pauni 100 milioni ya kupiga jeki kikosi chake kuelekea msimu wa dirisha la uhamisho Januari.
Masajini wapya ugani Old Trafford bila shaka watachochea baadhi ya wachezaji kuchujwa huku sita wakitazamiwa kuondoka.
Paul Pogba na Jesse Lingard pia wanaaminikan kuwa na hamu ya kuondoka huku Pogba akikataa kusaini mkataba mpya.
Lingard, kwa upande wake amepungukiwa kimchezo sabab ya ushindani, winga huyo akionekana kuondoka kama mchezaji wa bwerere iwapo United watashindwa kumpata mnunuzi wake Januari.
Wengine ni Anthony Martial, Diogo Dalot, na Donny van de Beek.
Licha ya ubabe wake Old Trafford, Martial ameshindwa kutimiza wajibu wake na sasa atatupwa sokoni United wakijaribu kurejesha pesa walizolipa Monaco kupata huduma zake.
Wakati huo huo Van de Beek, amekuwa na wakati mgumu Theatre of Dreams, akisugua benchi msimu mzima akiwa na United.