Fri, 18 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu za Saudi Arabia zimeripotiwa kuanza mchakato wa kuvamia Arsenal kwa ajili ya kwenda kunasa huduma ya beki wa kati wa Kibrazili, Gabriel Magalhaes.
Klabu hizo zinazoshiriki Saudi Pro League zimekuwa bize kwenye dirisha hili la majira ya kiangazi kusajili wachezaji wenye majina makubwa kutoka Ulaya ili wakacheze kwenye ligi yao.
Klabu za soka za Ulaya zipo kwenye mashaka makubwa kutokana na dirisha la usajili la Saudi Arabia kuwa wazi hadi Septemba 20.Gabriel amekuwa mchezaji muhimu sana kwenye kikosi cha Arsenal na mkataba wake kwenye klabu hiyo utafika tamati Juni 2.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live