Mwamuzi wa kati, Hussein Athumani kutoka Katavi na mwamuzi msaidizi namba mbili, Godfrey Msakila wa mkoani Geita wameondolewa kwenye ratiba ya waamuzi kwa mizunguko mitatu (3) kwa kosa la kushindwa kutafsiri vema sheria za mpira wa rniguu katika mchezo wa Young African SC na Mbeya City uliochezwa kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa Februari 5, 2022.
Mwamuzi wa kati, Hussein Athumani kutoka Katavi na mwamuzi msaidizi namba mbili, Godfrey Msakila wa mkoani Geita wameondolewa kwenye ratiba ya waamuzi kwa mizunguko mitatu (3) kwa kosa la kushindwa kutafsiri vema sheria za mpira wa rniguu katika mchezo wa Young African SC na Mbeya City uliochezwa kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa Februari 5, 2022. Hali kadhalika mwamuzi wa kati Ahmada Simba kutoka Kagera, aliechezesha mchezo kati ya Simba na Tanzania Prisons pia amekumbana na kadhia ya kuondolewa kwenye ratiba ya waamuzi kwa mizunguko mitatu (3)kwa kosa la kushindwa kutafsiri vyema sheria za mpira wa miguu katika mchezo wa Simba dhidi ya Prisons uliopigwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa Februari 3.