Kwa mjibu wa gazeti la l’Équipe ambalo huchapisha Mishahara kuhusu wachezaji wanaolipwa Mishahara ya juu nchini Ufaransa, Mchezaji Kylian Mbappé ameendelea kuongoza katika orodha akilipwa euro milioni 6 kwa mwezi huku Mwafrika Mmorocco Ashraf Hakimi, akipata euro 738,000.
PSG ipo katika timu kumi za kwanza zinazolipa vizuri kwenye Ligi Kuu nchini Ufaransa.
Mbali na Ufaransa, ni Mnigeria Victor Osimhen ambaye anatawala orodha ya wachezaji wanaolipwa zaidi katika michuano ya Italia akilipwa euro milioni 1.5 huku Mmisri wa Liverpool, Mohamed Salah akipata Euro milioni 1.7 kwa mwaka.
Waafrika 5 wanaolipwa zaidi Ligue 1
1. Achraf Hakimi (PSG, Morocco) €738,600
2. Pierre-Emerick Aubameyang (OM, Gabon) €650,000
3. Geoffrey Kondogbia (OM, Jamhuri ya Afrika ya Kati) €450,000
4. Isamaïla Sarr (OM, Senegal) €390,000
5. Said Benrahma (Olympique Lyonnais, Algeria) €350,000