Tue, 12 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Serikali imesema viti vyote 60,000 katika Uwanja wa Benjamini Mkapa vitaondolewa na kuwekwa vipya.
Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa ameeleza hatua hiyo ni mwendelezo mpango wa ukarabati wa uwanja huo ambao utakamilika mwezi Agosti mwaka huu.
“Kama kutakuwa na ongezeko la muda tutawajulisha,”amesema Msigwa.
Akizungumza na Wasafi FM, Msigwa amesema baada ya kukamilika uwanja huo utatengenezewa utaratibu mpya wa kiuongozi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live