Ofisa Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Azam Fc Hasheem Ibwe ameonyesha kufurahia matokeo ya juzi baada ya kutoka sare na Simba kwa kufungana goli 1 - 1 katika mwendelezo wa Ligi Kuu Soka Tanzania Bara.
Hashim Ibwe amesema hayo wakati akizungumzia mchezo huo wa juzi ambao ulimalizika kwa sare ya bao 1-1 katika Dimba la CCM Kirumba jijini Mwanza.
“Kama ilivyo kwa Sopu na Yanga, ndivyo hivyo ilivyo kwa Prince Dube na Simba kwani hawana mpango wa kumaliza tofauti zao.”
Hashim Ibwe ametamba kwa kusema kuwa wataendelea kumtumia Dube kwenye michezo mikubwa huku akiweka wazi uwepo wa James Akaminko katika klabu hiyo.