Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Vita ya Mayele, Saido yahamia Tanga

Mayele Na Saido S Vita ya Mayele, Saido yahamia Tanga

Mon, 12 Jun 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Huko mtaani hadi sasa mjadala ni ishu ya Tuzo ya Mfungaji Bora wa Ligi Kuu Bara, baada ya Fiston Mayele wa Yanga na Saido Ntibazonkiza wa Simba kufungana kwa kila mmoja kufunga mabao 17, huku Bodi ya Ligi (TPLB) ikishindwa kuainisha kanuni za msimu huu zinaamua jambo hilo.

Mashabiki wa Yanga wanaamini Mayele anastahili kubeba tuzo hiyo, huku wale wa Simba wakimpigia upatu Saido aliyesajiliwa Msimbazi katika dirisha dogo akitokea Geita Gold alikofunga mabao manne na kuasisti mara sita kabla ya kuongeza mabao mengine 13 na asisti sita pia akiwa na Wekundu.

Sasa kama hujui ni kwamba vita ya mastaa hao sasa imehamia kwenye tuzo za msimu zinazotarajiwa kutolewa leo jijini Tanga, hafla itakayofanyika mara baada ya mechi ya fainali ya Kombe la Shirikisho (ASFC) itakayozikutanisha Yanga na Azam FC kwenye Uwanja wa Mkwakwani, jijini humo.

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) linalosimamia tuzo hiyo kupitia Kamati ya Tuzo imepeleka hafla hizo Tanga na kuipanga ifanyike muda mfupi tangu kupigwa kwa mechi hiyo ya fainali ya ASFC kutokana na muingiliano wa kalenda ya FIFA inayohusisha mechi za kimataifa kwa timu za taifa.

Baadhi ya nyota wa timu za Ligi Kuu walioitwa na timu zao wakiwamo wale wa Tanzania, Taifa Stars na nyota wa kigeni wanatakiwa kuwahi kambi za timu zao, kwa ajili ya mechi za raundi ya tano ya kuwania kufuzu fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) 2023 zitakazopigwa kati ya Juni 14-20.

Stars yenyewe inatarajiwa kuikaribisha Niger kwenye pambano litakalopigwa Juni 18 ambapo timu hiyo ya Tanzania inahitaji ushindi ili kujiweka pazuri kwa ajili ya kufuzu fainali hizo za Ivory Coast.

MAENEO MANNE MAGUMU

Achana ishu za mechi za kufuzu Afcon 2023, unaambiwa kwenye tuzo hizo za msimu huu ambao majina ya wanaowania yalitangazwa wiki kadhaa zilizopita kuna maeneo manne magumu ikiwamo kuibuka upya kwa vita ya Mayele na Saido kwenye vipengele viwili tofauti.

Vipengele vinne vinaonekana kutotabirika katika uwaniaji wa tuzo hizo za msimu huu, ambazo washindi wake watatangazwa leo ni ile ya Mchezaji Bora, Kiungo Bora, Beki Bora na ile ya Mfungaji Bora wa msimu vipengele vinne ambavyo vinaonekana kuteka hisia za wengi katika utoaji wa tuzo hizo msimu huu.

Kiwango bora kilichoonyeshwa na walioteuliwa kugombea ushindi wa tuzo, unafanya wengi wasubiri kwa hamu kuona nani watakaibuka washindi katika vipengele hivyo.

Vita kubwa inaonekana ipo katika tuzo ya mchezaji bora ambayo inawaniwa na Fiston Mayele na Djigui Diarra wa Yanga, Saido Ntibazonkiza na Mzamiru Yassin (Simba) na Bruno Gomes wa Singida Big Stars.

Mayele amekuwa na msimu bora ndani ya kikosi cha Yanga akiifungia mabao 17 yaliyochangia itwae ubingwa wakati Diarra amekuwa nguzo imara golini, akiongoza katika kucheza idadi kubwa ya mechi bila kuruhusu mabao.

Wakati Saido Ntibazonkiza akionyesha kiwango bora katika kufumania nyavu na kupiga pasi za mwisho akiwa amehusika na mabao 29 ambapo amefunga 17 na kupiga asisti 12, Mzamiru Yassin ameonyesha kiwango bora katika safu ya kiungo ya Simba.

Kwa upande wa Bruno, amekuwa uti aa mgongo wa Singida United hasa katika kuichezesha timu na kufunga mabao ambapo amepachika idadi ya mabao tisa.

Katika tuzo ya kiungo bora, Mzamiru, Bruno, Saido wakiungana na Clatous Chama na Aziz Ki watanogesha ushindani wa kuwania mshindi wa kipengele hicho.

Wakati Chama akibebwa na idadi kubwa ya pasi za mwisho ambapo amepiga 14, Aziz Ki anabebwa na mabao yake ambayo ni nane huku akipiga pasi za mwisho tatu.

Bakari Mwamnyeto na Dickson Job walioonyesha kiwango bora cha kuilinda timu katika kikosi cha Yanga msimu huu kilichoruhusu mabao 18, watakuwa wakiwania tuzo na Enock Inonga, Mohamed Hussien na Shomari Kapombe ambao wameiongoza timu yao kuruhusu mabao 17 pia.

Tuzo zingine ambazo zinaonekana zitakuwa zinapasua kichwa wengi na kuleta hamu ya kufahamu ni nani anaweza kuibuka mshindi ni ile ya mwamuzi bora na refa bora msaidizi, mchezaji bora wa Kombe la Shirikisho la Azam, kamishina bora na mchezaji bora wa Ligi Kuu ya Wanawake.

Djigui Diarra anaonekana kuwa katika nafasi nzuri ya kuibuka mshindi wa tuzo ya kipa bora kama ambavyo Omari Malule anaonekana kuwa katika nafasi nzuri ya kuwa meneja bora wa uwanja.

TUZO ZILIVYO

KOMBE LA ASFC

KIPA BORA

Benedict Haule (Singida)

Djigui Diarra (Yanga)

Abdulai Iddrisu (Azam)

MCHEZAJI BORA

Prince Dube (Azam)

Fiston Mayele (Yanga)

Abdul Suleiman (Azam)

Bakari Mwamnyeto (Yanga)

Clement Mzize (Yanga)

MFUNGAJI BORA

Andrew Simchimba-7 (Ihefu, iliyotolewa)

Clement Mzize - 6 (Yanga)

Abdul Suleiman- 3 (Azam)

LIGI KUU WANAWAKE

KIPA BORA

Najiath Abbas (JKT Queens)

Winfrida Jedah (Fountain Princess)

Gelwa Yona (Simba Queens)

CHIPUKIZI BORA

Winfrida Charles (Alliance Girls)

Winfrida Gerald (Fountain Princess)

Jackline Shija (JKT Queens)

MCHEZAJI BORA

Donisya Minja (JKT Queens)

Jentrix Shikangwa (Simba Queens)

Amina Bilal (Yanga Princess)

KOCHA BORA

Ally Ally (JKT Queens)

Juma Hussein (Fountain Princess)

Charles Lukula (Simba Queens)

KIKOSI BORA

Kitatajwa leo

MFUNGAJI BORA

Jentrix Shikangwa (Simba Queens)

TIMU YENYE NIDHAMU

Amani Queens

JKT Queens

Alliance Queens

MWAMUZI BORA

Jonesia Rukyaa-Kagera

Tatu Malogo- Tanga

Esther Adalbert- Singida

MWAMUZI MSAIDIZI BORA

Janeth Balama- Iringa

Glory Tesha- Dar

Zawadi Yusuph- Dar

LIGI KUU BARA

MCHEZAJI BORA

Mzamiru Yassin (Simba)

Fiston Mayele (Yanga)

Bruno Gomes (Singida)

Djigui Diarra (Yanga)

Saido Ntibazonkiza (Geita/ Simba)

KIPA BORA

Aishi Manula (Simba)

Djigui Diarra (Yanga)

Benedict Haule (Singida)

BEKI BORA

Dickson Job (Yanga)

Henock Inonga (Simba)

Bakar Mwamnyeto (Yanga)

Shomari Kapombe (Simba)

Mohamed Hussein (Simba)

KIUNGO BORA

Bruno Gomes (Simba)

Mzamiru Yassin (Simba)

Stephane Aziz KI (Yanga)

Clatous Chama (Simba)

Saido Ntibazonkiza (Geita/Simba)

KOCHA BORA

Nasreddine Nabi (Yanga)

Hans Pluijm (Singida)

Roberto Oliveira (Simba)

MENEJA BORA UWANJA

Omari Malule (Highland Estate, Mbeya)

Hassan Simba (Liti, Singida)

Amri Juma (Azam Complex)

CHIPUKIZI BORA

Clement Mzize (Yanga)

Edmund John (Geita Gold)

Lameck Lawi (Coastal Union)

KIKOSI BORA

Kitatangazwa leo

TIMU YENYE NIDHAMU

KMC

Ruvu Shooting

Tanzania Prisons

MWAMUZI BORA

Jonesia Rukyaa (Kagera)

Tatu Malogo (Tanga)

Ramadhan Kayoko (Dar)

Mwamuzi Msaidizi Bora

Mohamed Mkono (Tanga)

Frank Komba (Dar)

Janeth Balama (Iringa)

SETI BORA WAAMUZI

Simba v Yanga

Jonesia Rukyaa

Mohamed Mkono

Janeth Balama

Tatu Malogo

Simba v Azam

Abdi wajihi

Arnold Bugado

Martin Mwalyaje

Isihaka Mwalile

Geita Gold v Dodoma Jiji

Jonesia Rukyaa

Zawadi Yusuph

Athuman Rajabu

Ally Simba

KAMISHNA BORA

Isaac Munisi

Hosea Lugano

Said Mankilingo

MCHEZO WA KIUNGWANA

Saido Ntibazonkiza (Geita/ Simba)

Jean Baleke (Simba)

Pape Ousmane Sakho (Simba)

BAO BORA

Litafahamika leo

MFUNGAJI BORA

Fiston Mayele-17 (Yanga)

Saido Ntibazonkiza- 17(Geita/Simba)

TUZO ZA UTAWALA

TUZO YA HESHIMA YA WPL

Mshindi atatangazwa leo

MCHEZAJI GWIJI

Mshindi atatangazwa leo

TUZO YA HESHIMA

Mshindi atatangazwa leo

TUZO YA RAIS

Mshindi atatangazwa siku ya sherehe

LIGI NYINGINE

Mchezaji Bora Championship

Edward Songo (JKT Tanzania)

John Budeba (Mashujaa)

Fabrice Ngoy (Kitayosce)

MCHEZAJI BORA FIRST LEAGUE

Ramadhan Athuman (Rhino Rangers)

Abdulrahman Mapande (Cosmopolitan)

Tungu Kashinje (Stand United)

MCHEZAJI BORA U20

Lamdaki Chasambi (Mtibwa Sugar)

William Mwani (Mbeya Kwanza)

Clement Mzize (Yanga)

MCHEZAJI BORA SOKA UFUKWENI

Ligi bado haijachezwa

WASHINDI MSIMU ULIOPITA

MCHEZAJI BORA

Yannick Bangala (Yanga)

KIUNGO BORA

Yannick Bangala (Yanga)

KIPA BORA

Djigui Diarra (Yanga)

MFUNGAJI BORA

George Mpole (Geita Gold)

BEKI BORA

Henock Inonga (Simba)

Mwanaspoti. Kata k

Chanzo: www.tanzaniaweb.live