Sat, 18 Feb 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Vipers ya Uganda imebanwa uwanja wao wa nyumbani nchini Uganda baada ya kutoka suluhu (0-0) dhidi ya Horoya AC ya Guinea.
Matokeo hayo yanaifanya Horoya kuwa na pointi 4 katika kundi C ambalo wapo na Simba na Raja Casablanca.
Vipers katika mchezo wa leo wamejikuta wakimaliza mchezo wakiwa pungufu baada ya mchezaji wao I. Mubiru kuoneshwa kadi nyekundu dakika ya 78.
Simba ndio Timu pekee kutoka kundi C ambayo haina alama mpaka sasa na wapo Uwanjani kupepetana na Raja Casablanca.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live