Tue, 3 Sep 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Galatasaray ya nchini Uturuki imekamilisha usajili wa mshambuliaji Victor Osimhen raia wa Nigeria kwa mkopo wa msimu mzima mpaka Juni 2025 akitokea Napoli.
Kwenye mkataba huo Galatasaray itawajibika kulipa mshahara wote wa nyota huyo, lakini miamba hiyo ya Uturuki haitakuwa na chaguo wala jukumu la kumchukua jumla mwisho wa msimu.
Mkataba wa Osimhen na Napoli una kifungu cha 'release clause' cha Euro Mil 75 na utafikia ukomo Juni 2026 huku miamba hiyo ya Italia ikiwa na chaguo la kumuongezea mpaka 2027.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live