Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Van Nistelrooy kurejea Man United

Ruud Van Nistelroy Van Nistelrooy kurejea Man United

Tue, 25 Jun 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mshambuliaji wa zamani wa Manchester United, Ruud van Nistelrooy, anaweza kurejea Manchester United kama sehemu ya wakufunzi wa Erik ten Hag huko Old Trafford.

Mholanzi huyo mwenye umri wa miaka 47 anaweza kuchukua nafasi ya msaidizi wa Ten Hag, Mitchell van der Gaag au kocha wa mbele Benni McCarthy, ambaye mkataba wake unamalizika mwishoni mwa mwezi.

Van Nistelrooy aliichezea United kati ya 2001 na 2006, akifunga mabao 150 katika mechi 219 chini ya Sir Alex Ferguson.

Hata hivyo bado kuna ukakasi kweye mpango huo, kwani Van Nistelrooy pia yuko kwenye mazungumzo na klabu ya Burnley ili kuchukua nafasi ya ukocha iliyoachwa na Vincent Kompany aliyejiunga na Bayern Munich mwezi uliopita.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live