Mchezo wa Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika kati ya Simba dhidi ya Orlando Pirates unaotarajiwa kuchezwa Aprili 17, 2022 kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa, waamuzi watatumia msaada wa video [Video Assistant Referee-VAR] pale itakapobidi kutumia ili kuhakikisha maamuzi yanakuwa sahihi.
Tayari orodha ya waamuzi wa mchezo huo imeshajulikana sambamba na wale watakao ongoza VAR.
Orodha ya waamuzi hao ni kama ifuatavyo;
Referee: Haythem Guirat (Tunisia) Assistant Referee 1: Khalil Hassani (Tunisia) Assistant Referee 2: Samuel Pwadutakam (Nigeria) Fourth Official: Sadom Selmi (Tunisia) Video Assistant Referee: Ahmed Elghandour (Misri) Assistant VAR: Youssef Wahid Youssef Misri.
Tayari kila anayehusika na mchezo huo ikiwa ni pamoja na vilabu, wameshapewa taarifa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) juu ya uwepo wa matumizi ya VAR kwenye mchezo huo.
VAR itatukika kwenye mechi zote za timu zilizofuzu hatua ya Robo Fainali ya michuano ya CAF.