Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Uteuzi wa Mo Dewji Simba SC ni batili

Abdul Akara Uteuzi WaMo Uteuzi wa Mo Dewji Simba SC ni batili

Sun, 5 Mar 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mchambuzi Abdulaziz Mrisho akizungumzia uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Simba SC uliofanywa na mwekezaji Mohammed Dewji kupitia TBC amesema hakuna kifungu Kisheria na kikatiba kinachompa Mo mamlaka ya kumteua Try Again.

Amebainisha kuwa wajumbe 8 huiwakilisha Simba SC kwenye Bodi ya Wakurugenzi, ambapo wajumbe 6 huchaguliwa na wawili wa huteuliwa ambapo mmoja kati yao atachaguliwa kama Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi. Hapa ndipo unaona mwenye mamlaka ya kumchagua Try Again ni Murtaza Mangungu na sio Mo Dewji.

“Katiba ya Simba Ibara ya 27 inampa mamlaka Mwenyekiti Simba SC aliyechaguliwa na Wanachama kuteua mjumbe wa bodi miongoni mwa upande wa asilimia 51 ambaye ni Salim Try Again baada ya hapo akapewa nafasi ya kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi.”

“Kikatiba hakuna kifungu kinachompa mamlaka Mohammed Dewji kuteua Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya klabu ya Simba anachaguliwa na wajumbe wa bodi ya Wakurugenzi wa klabu.”

Bodi ya Wakurugenzi ya Simba SC ndio yenye mamlaka ya kupitisha nani awe Mwenyekiti. Kitendo cha Mo kumteua Try Again kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Simba SC hakipo kisheria na kikatiba.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live