Nchini Rwanda mabishano yanaongezeka baada ya mchezaji kutoka klabu moja kuu ya nchi hiyo kutumia ishara sawa na timu ya soka ya DRC wakati wa Michuano ya AFCON kukemea ukimya unaozingira mzozo Mashariki mwa nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Mkono mmoja mbele ya mdomo na vidole viwili vya mkono mwingine kichwani ni kwa ishara hii kwamba mchezaji wa Kongo Héritier Luvumbu Nzinga alisherehekea bao wakati wa mechi kati ya klabu yake ya Rayon Sports na Polisi FC mjini Kigali.
Kitendo kilichotajwa sana kwenye mitandao ya kijamii na watumiaji wengi wa mtandao wa Rwanda wakiitaka klabu hiyo kumsimamisha mchezaji huyo na kufikia hatua ya kuomba afukuzwe nchini na kukosoa kitendo cha kuchanganya michezo na siasa.
Rayon Sports ilisema “imesikitishwa na tabia mbaya” ya mwanasoka huyo katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyochapishwa Jumatatu alasiri, ikitoa wito kwa washiriki wa timu kuwa na nidhamu ndani na nje ya uwanja.