Sun, 31 Oct 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mashetani wa Jiji, timu ya Manchester United imezinduka na kuichapa Tottenham Hotspur mabao 3-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Tottenham Hotspur Jijini London.
Mabao ya Manchester United, yamefungwa na Cristiano Ronaldo dakika ya 36, Edinson Cavani dakika ya 64 na Marcus Rashford dakika ya 86.
Kwa ushindi huo, Manchester United imefikisha pointi 17, mbili zaidi ya Tottenham baada ya timu zote kucheza mechi 10.
Ushindi huo angalau umeshusha presha kwa Meneja wa kikosi hicho, Ole Gunner Solskjaer ambae awali alipewa mechi tatu kunusuru kibarua chake.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live