Kocha wa Manchester United Ralf Rangnick amesema wachezaji wake takribani wote wamerejea kwenye kikosi cha timu hiyo baada ya kushindwa kujiunga nayo kutokana na hofu ya maambukizi ya virusi vya Covid-19.
Kuibuka kwa kirusi kipya cha Omicron kulipelekea mechi mbili za Man United kuahirishwa, mtanange wa Brentford na ule wa Brighton.
Kuelekea mchezo wa Jumatatu dhidi ya Newcastle United Disemba 27, kocha Rangnick amesema atakosa huduma ya kiungo mshambuliaji wa kimataifa wa Ufaransa Paul Pogba ambaye ni majeruhi.
“Leo ilikuwa ni siku ya tatu ya mazoezi, tulikuwa na wachezaji 25, ni Pogba pekee ambaye hakuwa sehemu ya mazoezi”. Alisema Rangnick