Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Unajua kwa nini Cristiano Ronaldo hamiliki Akaunti ya You Tube?

Ronaldoooooooooooo Unajua kwa nini Cristiano Ronaldo hamiliki Akaunti ya You Tube?

Mon, 10 Jun 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Umewahi kujiuliza kwanini @cristiano hana Youtube Channel? Inadaiwa kwamba Cristiano Ronaldo hawezi kumiliki Youtube Channel kwa sababu itakuwa vigumu Youtube kumlipa kwani wanaweza kuingia kwenye hasara kubwa kutokana na nguvu ya ushawishi aliyonayo, huenda video zake zikavunja rekodi, zikatazamwa zaidi, hivyo amezuiliwa kumiliki Channel ya Youtube.

"Youtuber" maarufu Duniani Mr Beast ana zaidi ya Subscribers Million 200, ametumia miaka 13 kufikisha idadi hiyo ila inakadiriwa kwamba Ronaldo ana uwezo wa kufikisha Subscribers hao ndani ya miaka mitatu tu.

Ronaldo amewahi kufungua ukurasa wa TikTok, kabla ya masaa 24 alikuwa amepata wafuasi milioni 4, Likes milioni 10, TikTok wakaamua kufunga Account yake, ingawa baadhi ya Watu wanakanusha dai hili wanadai kwamba aliyefungua account hiyo siyo Ronaldo halisi, ni mtu mwingine ila alitumia jina la Ronaldo ndiyo maana TikTok wakafunga account hiyo.

Ronaldo ndiye binadamu anayeongoza kwa wafuasi wengi Instagram, ana zaidi ya Wafuasi milioni 631.

Je, unakubaliana na watu wanaodai kwamba Ronaldo hawezi kulipwa na Youtube, na akilipwa basi Youtube itafilisika?

Chanzo: www.tanzaniaweb.live