Tue, 25 Oct 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Aston Villa imethibitisha kumteua kocha wa zamani wa Arsenal Unai Emery kuwa kocha mkuu klabuni hapo.
Emery amelazimika kuvunja mkataba na klabu yake ya Villareal na kutua klabuni hapo kuchukua mikoba ya Steven Gerrard.
Hata hivyo Emery atalazimika kusubiri mpaka Novemba Mosi kuanza kazi Villa kutokana na shida ya kupata kibali cha kufanya kazi UK.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live