Mon, 16 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Uongozi wa ‘klabu’ ya Manchester United unatarajia kuongeza ulinzi katika mchezo ujao dhidi ya Copenhagen katika ‘ligi’ ya mabingwa ulaya kwenye mchezo utakaofanyika Uwanja wa OldTrafford ili kudhibiti mashabiki wanaodaiwa kupanga kufanya vurugu.
Hiyo nikutokana na uongozi wa ‘timu’ hiyo kugoma kuiuza ‘klabu’ ya Man United wiki iliopita.
Inadaiwa kuna kundi la mashabiki waliochukizwa na uamuzi wa familia ya Glazer kutoiuza ‘klabu’ hiyo wakiamini uwekezaji wao haunufaishi ‘timu’ bali unawabeba wao wawekezaji binafsi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live