Kuelekea Michuano ya Shirikisho CAF Confederation Cup 24/25 timu ya Uhamiaji FC ya Zanzibar itacheza Michezo yake yote ya awali nchini Libya.
Taarifa ya Uhamiaji FC Imesema Kumefanyika Mabadiliko ya Muda na Kiwanja Hivyo Kuanzia sasa Umma Unajuzwa Kwamba:-
Uhamiaji Vs Al Ahly Tripoli
Tripoli Stadium, Libya
2,00 Usiku 18 Agosti 2024
Al Ahly Tripoli Vs Uhamiaji
Tripoli Stadium, Libya
4:00 Usiku 23 Agosti 2024.
Sababu za Mabadiliko hayo bado hazijawekwa bayana.Isipokuwa Uongozi wa Klabu ya Uhamiaji FC Umesema ni Makubaliano ya Pande Mbili yamefanyika, pia Utakuwa Wasaa mzuri kuweza Kuimarika Vema Kuelekea Msimu 24/25 kwa Kupata safari hii ya nje ya nchi.
Ikumbukwe :- Mshindi wa Jumla kati ya Uhamiaji FC au Al Ahly Tripoli atakutana na Klabu ya Simba Katika Michuano hii ya Shirikisho.