Tue, 21 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Baada ya ukaguzi wa Marekebisho ya Uwanja wa Mandela (Namboole), Shirikisho la soka barani Afrika CAF wameiruhusu Uganda kuanza kucheza mechi zao nyumbani.
Kwa mjibu wa CAF, Uwanja huo umekidhi vigezo vya CAF na FIFA kwa ajili ya kupokea mechi za kimataifa.
Hivyo, Uganda atacheza nyumbani mwezi Juni na nchi za Algeria na Botswana katika kusaka tiketi ya kufuzu kombe la Dunia 2026.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live