Huwezi kulizungumzia soka la Ulaya kwasasa bila kuitaja Ufaransa, hawa wamefika fainali ya kombe la Dunia mara mbili mfululiza, wakibeba mara moja na kupoteza mara moja mbele ya Argentina.
Ufaransa ni kama wamelitawala kwa sasa soka la Dunia na Ulaya kupitia kampeni yao ya Importation of Talents, nyota wengi kutoka Afrika ambao wanaonekana kuwa na vipaji basi wanapata nafasi ya kuwatumikia.
Hivi ikitokea kile alichokisema Mourinho kuwa kila mchezaji akalitumikie Taifa lake la asili Ufansa wataendelea kulitawala soka ?
Leo tena tutakuwa tunautazama Umoja wa Mataifa ukikipiga dhidi ya Gibraltar saa 4:45 usiku kwenye kampeni ya kusaka tiketi ya kufuzu fainali za Euro