Uwanja wa Stadium 974 ni moja kati ya viwanja nane vitakavyotumika kwenye michuano ya fainali za kombe la dunia 2022 nchini Qatary.
Uwanja huo ambao ulisanifiwa na msanifu Fenwick Iribarren raia wa Hispania akishirikiana na Schlaich Bergermann Partner na mshauri mradi Hilson Moran, upo Doha ambapo umejengwa kutokana na Makontena 974.
Zamani ulifahamika kama uwanja waRas Abu Aboud, ambao una uwezo wa kubeba mashabiki 40,000 na tayari umekamilika.
Kutengenezwa kwa makontena hayo kuna malengo mengi ikiwemo kupunguza gharama za za ujenzi na maji kwa asilimia 40 ikilinganishwa iwapo ungejengwa kwa saruji.