Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Uchambuzi EPL: Liverpool vs Leicester City

Liv Leic liver wataikaribisha Licester City

Thu, 10 Feb 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Liverpool na Leicester City wanajitupa dimbani kwaajili ya muendelezo wa Ligi ya Premia katika dimba la Anfield siku ya leo Alhamisi.

Vijana wa Brendan Rodgers wanakuja kwenye mchezo huu wakiwa na kumbukumbu ya kipigo kikali kutoka kwa Nottingham Forest kwenye michuano ya FA Cup wakati Liverpool wakiiadhibu Cardiff City katika raundi ya 5 ya FA Cup.

Taarifa ya Timu

Divock Origi amerejea katika mazoezi kamili baada ya tatizo la goti, vile vile Joe Gomez na Alex Oxlade-Chamberlain wamemaliza vipindi vyao vya kutengwa baada ya kukutwa na maambukizi COVID-19, lakini Jordan Henderson anauguza tatizo dogo la mgongo.

Diaz anaweza kucheza kwa mara ya kwanza kwa majogoo wa Anfield baada yakusajiliw wakati wa dirisha la Januari.

Elliott ni kama hatocheza kwenye mtanange wa leo lakini Thiago Alcantara na Fabinho wote wanatazamia kurejea dhidi ya Leicester City.

Kwa upande wa The Foxes hawatakuwa na mchezaji wao Namplays Mendy ambaye pia alitajwa kwenye Bora XI ya AFCON 2021 huenda akachukua muda wa kupumzika kabla ya kurejea kwenye kikosi cha kwanza.

Jonny Evans, Timothy Castagne, Jamie Vardy, Ryan Bertrand na Wesley Fofana wote wamesalia nje ya mechi ya leo kutokana na jeraha, lakini majeruhi wa wanatarajiwa kujiunga tena na mazoezi ya timu wiki ijayo.

Kikosi cha Liverpool Kinachoweza kuanza: Alisson; Alexander-Arnold, Matip, Van Dijk, Robertson; Henderson, Fabinho, Thiago; Jota, Firmino, Diaz

Kikosi cha Leicester City Kinachoweza kuanza: Schmeichel; Pereira, Vestergaard, Soyuncu, Thomas; Ndidi, Tielemans; Albrighton, Maddison, Daka; Iheanacho

Chanzo: www.tanzaniaweb.live