Thu, 30 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Timu ya taifa ya Ujerumani imekutana na kipigo cha bao 3-2 dhidi ya Ubeligiji katika mchezo wa kirafiki uliochezwa Ujerumani mchezo ulichezwa katika uwanja wa RheinEnergie mji wa Köln.
Matokeo hayo yanamfanya kocha Domenico Tedesco wa Ubelgiji kushinda mechi mbili za awali kufuatia kuichukua timu baada ya Kombe la Dunia.
Mabao kwa Ubeligiji wageni yamefungwa na winga wa Atletico Madrid Yannick Carrasco, Romelu Lukaku na Kevin de Bruyne wakati wenyeji Ujerumani wamepata bao zao kupitia kwa Niclas Fullkrug (penalti) na kiungo mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Serge Gnabry.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live