Thu, 1 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Timu ya Taifa ya Ubelgiji imefungashiwa virago hatua ya Makundi michuano ya Kombe la Dunia inayoendelea nchini Qatar.
Ubelgiji imeondoshwa baada ya kulazimishwa sare ya bila kufungana na Croatia na kuacha mshangao mbele ya macho ya wapenda kandanda Duniani kutokana na kikosi chake kusheheni nyota wengi wanaotamba katika Ligi mbalimbali barani Ulaya.
Ubelgiji ilipangwa kundi F sambamba na timu za Morocco ambayo imemaliza kinara, Croatia iliyomaliza nafasi ya pili pamoja na Canada.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live