Klabu ya USM Alger ya nchini Algeria imenyakua Kombe la Caf Super Cup baada ya kuilaza Al Ahly kwa bao 1-0, mchezo uliopigwa nchini Saudi Arabia usiku wa Ijumaa.
Zinedine Belaid alifunga bao la ushindi katika kipindi cha kwanza kwa mkwaju wa penalti baada ya VAR kuamua katika kipindi cha kwanza.
Bao la ushindi kipindi cha kwanza lilionekana kuwa gumu huku timu ya Algeria ikijilinda kwa uthabiti na kuwazuia mabingwa wa Caf Champions League ambao walikuwa wanatawala muda wote wa mchezo.
Ikumbukwe kuwa, USM Alger ndiye mabingwa wa Kombe la Shirikisho Afrika na waliibeba ubingwa huo kwa kanuni ya bao la ugenini baada ya kulingana mabao na Yanga Sc kwenye mchezo wa fainali huju Zinedine Belaid akifunga bao dhidi ya Yanga.
Timu hiyo ya Misri (Ahly), mabingwa wa Ligi ya Mabingwa Afrika waliorekodi rekodi ya Caf walikosa fursa ya kutwaa mataji matatu ya kihistoria.
Sasa wanaelekeza nguvu zao kwenye kutetea ligi, Ligi ya Mabingwa Afrika na sasa Ligi ya Soka Afrika (Africa Football League) ambapo wanakutana na Simba Sc katika robo fainali.