Sun, 17 Oct 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wekundu wa Msimbazi, Simba SC wako mbele kwa magoli 2-0 dhidi ya wenyeji Jwaneng Galaxy ya Botswana.
Simba inacheza mchezo wa raundi ya kwanza kuwania kufuzu kwa hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika.
Kwa namna Simba ilivyoanza mchezo kwa kasi ni dhahiri wamepania kufanya jambo mapema.
Magoli ya msimbazi yamefungwa na nahodha wao John Bocco dakika za 2' na 6' ya mchezo na hivi sasa ni dakika ya 10.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live