Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Ulaya UEFA limeitisha mkutano wa dharura siku ya ijumaa kutathmini kitendo cha Urusi kuivamia nchi ya Ukraine ikizingatiwa Fainali ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya ilipangwa kuchezwa nchini Urusi Mei mwaka huu katika Dimba la Saint Petersburg.
Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Ulaya UEFA limeitisha mkutano wa dharura siku ya ijumaa kutathmini kitendo cha Urusi kuivamia nchi ya Ukraine ikizingatiwa Fainali ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya ilipangwa kuchezwa nchini Urusi Mei mwaka huu katika Dimba la Saint Petersburg. "Kutokana na hali iliyopo na inayoendelea baina ya Urusi na Ukraine katika kipindi cha saa 24 zilizopita, Rais wa UEFA ameamua kuitisha mkutano wa dharura wa Kamati ya Utendaji siku ya Ijumaa 25 Februari, kwa ajili ya kutathmini hali hiyo na kuchukua maamuzi yanayofaa" ilisema taarifa ya UEFA.